Thursday, December 20, 2007

HII NI KWA WOTE AU SIOO?

Kutokana na yale maombi niliyowaambia hapo awali huyu alikuwa anataka kujua historia ya waigizaji Angelina Jolie na brad Pitt.Kwa kifupi kwanza hawa ni mtu na mme wake.Leo ntakupa mambo muhimu ya Angelina na baadae Pitt.

Angelina Jolie Voight hilo ndilo jina lake kamili alizaliwa June 04,1975 Los Angeles,California USA.Baba yake anaitwa Jon Voight na mama yake Marcheline Bertrand.Pamoja na kuwa muigizaji wa muda sana pia alikuwa mwanamitindo.Angelina pia ni balozi wa umoja wa mataifa(UN)katika mambo ya wakimbizi.Anajulikana kwa majina mengine(Nickname) kama Angie,Catwoman,Ange&AJ.Angie ameigiza movie nyingi sana lakini baadhi ni Tomb Raider 2001&2003,Alexander 2004,Mr&Mrs Smith 2005,The Good Shepherd 2006,A Mighty Heart 2007 na mpya inayotamba sasa Beowulf 2007.Pia kuna baadhi ambazo zitatoka 2008 kama Kung Fu Panda,Wanted na zingine.Angeline ameshinda tuzo kama Showest 2000,Oscar 1999 na zingine nyingi tu.Ana mambo kibao lakini kwa ufupi ni hayo.Usikose issue za Brad Pitt.

WATU WANGU MNIWIE RADHI

Kwanza kabisa nilikuwa nataka kuwaomba msamaha watu kwa kutokuwa hewani kwa siku kazaa lakini kama nilivyowaambia tupo pamoja.Hii pia ni pamoja na mtu ambaye alikuwa anitaka kujua historia ya waigizaji maarufu huko Hoollywood,Mshikaji wangu nakwambia leo hii nitakupa vitu.Pia waweza kucheki hapa ili kupata vitu na nilipotolea maoni hayo.