Thursday, December 06, 2007
WAMJUA SALMA HAYEK WEWE MPWA WA OSAMA?
Huyu ni muigizaji mzuri na maarufu sana wa kike aliyejichukulia umaarufu mkubwa sana huko Hoolywood.Salma alizaliwa tarehe 02 september 1966, Coatzacoalcos, Veracruz, Mexco. Sasa ana umri wa miaka 41, na jina lake kamili ni hilo hilo Salma Hayek Jimeneaz.Mwana dada huyu ameigiza movie nyingi sasa ambazo kiukweli mimi mwenyewe nazikubali, Movie za 2007 ni kama Ugly Betty na Across the Universe.Movie zake ambazo hadi sasa zinatarajiwa mwaka 2008 ni Keep Coming Back na South of the Border na pia kuna pre-production zake za 2009 inaitwa Banda,La.Pia kuna tetesi kuwa Salma ni mpwa wa Osama Bin Laden,lakini pia inadaiwa kuwa ajawahi kuonana uso kwa uso na mjomba ake huyo. Usikose mambokibao yanakuja kama kawaida.
Wednesday, December 05, 2007
UNAMJUA MGUMU AMBAYE NI MCHESHI SANA?
Najua utakuwa unajiuliza maswali mengi sana kichwani mwako huyo ni nani haswa? Basi kama kawaida mtu wangu hapa ndo umefika. Jamaa ni boge la actor(muigizaji) ambaye ukiangalia movie zake za comedy(ucheshi) hautaacha kufurahi mwanzo mpaka mwisho na ikibidi waweza rudia tena kuangalia.Anajulikana kwa jina maarufu kama ICE CUBE pia ana majina mengine kama Westside Connection,N.W.A, Mshikaji amezaliwa tarehe 15 June 1969,Los Angeles,California,USA.Ice Cube pia ni rapper mkali sana toka miaka mingi jamaa amekuwa akifanya HipHop. Pia Ice ni mwandishi wa mashairi na mwongozaji wa filamu.Jina la kuzaliwa la Ice Cube ni O'Shea jackson.Ana movie nyingi sana lakini movie yake inayozungumziwa ni Are We Done Yet? amboyo ni ya mwaka huu 2007.Endelea kucheki na hii tovuti utazidi kupata vitu vingi vya Ice Cube na mastar wengine kibao.
Tuesday, December 04, 2007
WAZIJUA TOP 5 ZA MOVIE.COM ZA LEO
Hizi ni TOP 5
1.Enchanted
2.This Christmas
3.Beowulf
4.Awake
5.Hitman
Hizo ndio zinabamba kwenye box-office results ya movie.com
1.Enchanted
2.This Christmas
3.Beowulf
4.Awake
5.Hitman
Hizo ndio zinabamba kwenye box-office results ya movie.com
TUPO PAMOJA?
Hii nilikuwa nataka kuwa kumbusha wale wadau na wa wapenzi wa filamu hasa katika nchi zetu ambazo ndio kwanza zinaanza kuchipukia katika mambo ya filamu,tuwaunge mkono wasanii wetu kwa kununua kazi zao.Na pia kuwapinga na kuwafichua wale wachache wanao warudisha nyuma kwa kuwaibia wasanii kazi zao.
Monday, December 03, 2007
USIKONDE MTU WANGU.
Watu wangu wote ambao tupo pamoja msiwe na tabu kabisa kama unataka kumjua star mojawapo wa movie unaweza kunitumia maoni yako nami bila hiana ntakupa mambo pamoja na kila kitu.Basi waweza nitumia maoni na kumchagua star yeyote anayetaka kujua undani wake.Shwariii!
INAPENZA SANA AU SIO WATU WANGU?
Mwisho wa wiki iliyopita nilipata bahati ya jusikiliza mahojiano ya waigizaji maarufu a hapa Bongo(Tanzania) katika kituo kimoja maarufu pia hapa kwetu Tz cha television.Nilifurahi sana kusikia toka kwao wakisema sasa afadhali hata filamu zoa za kibongo afadhali zimeanza kuwalipa waigazaji hao.Ni jambo la faraja sana maana hio inamaanisha watanzania na watu wao wa jirani wameanza kupata muamko na fleva za movie za bongo. Hii pia ni pamoja na kuanza kupata majibu kwa maswali mengi tuliyokuwa tunajiuliza, pia waweza rudia mada iliyopita.Ushauri wa bure kutoka kwangu kwa wasanii hao wasibweteke na mafanikio hayo waliyo anza kuyapata tunahitaji sana na wao wajulikane kimataifa ili watuwakilishe kwa sana au sio?
Subscribe to:
Posts (Atom)