Friday, November 30, 2007
JE TUFANYAJE??
Mambo vipi watu wangu popote mlipo?Hilo swali nimelitoa kwenu ili tupate kujadili kuhusu jinsi ya kukuza soko la filamu sana sana katika nchi hazijapata maendeleo kivile.Kwa mfano mimi ni Mtanzania,na ukimuuliza Mtanzania yeyote yule anayeishi Tanzania atakwambi jinsi filamu zinavyotoka za kumwaga(nyingi mno) karibu kila siku iendyo kwa Mungu lakini kwa mtazamo tu soko la Tanzania bado lipo chini sana na sizani kama kuna filamu nyingine zinafika hata katika nchi jirani za Tanzania nikimaanisha Kenya na Uganda.Je filamu hizi hazina ubora wa kutosha au unaotakiwa au nini haswaa tatizo?Ndio nawauliza Je tufanyaje kukuza soko la nchi ambazo ziko kama Tanzania???
Thursday, November 29, 2007
VIPI UNAMJUA MKALI WA KUNG-FU??
Ebwana nadhani wale makini wamekwisha gundua huyo ni nani ambaye anataka kuzungumziwa au sio?Kwa wale ambao wanaanza kujiuliza uliza hii inukuwaje tena?huyu jamaa anazungumzia mkaliwa kung-fu na wakati wako kibao wanaigiza filamu kibao,Hilo nalijua lakini watu wangu ukimzungumzia huyu ninaye mzungumzia ni kiboko,basi kama bado mnaumiza vichwa wale wenye kuwa na wasiwasi wala msipate tabu sana.Hata hivyo kabla sijawataji jina lake nikikwambia hivi nadhani utanipata,jamaa ameigiza filamu kama Shaolin temple 1&2 hiyo ni mwaka 1982 na 1983 pamoja na 3 mwaka 1986,Born to Defence nayo mwaka 1986,zingine ni kama Fist of legend(1994) na nyingine nyinngi pia Romeo must die(2000),The One na Kiss Of The Dragon mwaka 2001.Hero(2002),Fearless(2006) na The Warlords War(2007).Hizo movie sio kama nimewatajia zote watu wangu ni baadhi tu ya filamu alizocheza.Namzungumzia JET LEE na majina mengine kibao kama Lian Jie Li,Lianjie Li,Jet Li Lianjie,Jet Lee Lin-kit. Hayo yote ni majina yake. Jamaa alizaliwa tarehe 26 April 1963,huko Beijing,China.Huyo ndio mkali wa Kung Fu,Usikose habari zake pamoja na wengine wengi kwenye hii hii Blog yako kali ya filamu pamoja na waigizaji wa filamu hizo au sio.Kuwamakini kaa mkao wa kula.
Wednesday, November 28, 2007
KWELI MGANGA HAJIGANGI?
Msishtuke watu wangu sio kwamba nataka kuzungumzia ya kimethali sana,Hapana!Nilikuwa nahitaji tu na nyinyi mnipe maoni yenu ausio?kama ni kweli mganga hajigangi sijui hii unaionaje wewe. Je umekwisha iona filamu(movie) ya HITCH iliyoigizwa na muigizaji maarufu sana mwenye vipaji lukuki,kama vile uchekeshaji pia ni mwimbaji n.k.Kama bado ujanipata namzungumzia nani basi huyo niWill Smith.Kwenye hii filamu ameigiza kama mtu aliyebobea katika mambo ya uelimishaji wa muahusino ya kimapenzi.Je yeye ataweza kujiimarisha na kudumisha muhusiona yake na girlfriend wake au atabakia kuwaelimisha wengine na yeye anabakia kushangaa shangaa?Hebu tafuta na uicheck hiyo imetulia.
Tuesday, November 27, 2007
SHWARI TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Nikizungumzia filamu au naweza sema movie ambazo zilitamba wakati fulani baadhi ya watu wanazo kumbuka wanaweza fahamu mimi nina rika gani hivi sasa.Lakini sio tabu sana hata ambao hawakuwepo muda huo wanaweza kuzitafuta movie hizo na kuziangalia zilivyokuwa zinarizisha.Ok msiwe na hofu wala na wasiwasi maana mtaanza kujiuliza ni zipi hizo movie jamaa anataka kuzungumzia.Poa unazikumbuka movie kama Commando ya Arnod,je Blood sport ambazo zilikuwa na mifululiza kadhaa(parts). Na zingine kibao ntazidi kuwakumbusha watu wanngu msikose basi au sio?/
KARIBUNI KATIKA BLOG MPYA YA FILAMU
Karibuni watu wote katika blog yenu mpya kabisa itakayokuwa inazungumzia kuhusu filamu mbalimbali pamoja na waigizaji wa filamu hizo. kama wewe ni mpenzi wa filamu mbalimbali basi sasa ondoa shaka maana mkombozi wako amekwisha wasili kwa sababu huta pitwa na habari za filamu bomba pamoja na wasanii au waigizaji wa filamu natumaini tuko pamona yap.
Subscribe to:
Posts (Atom)