Thursday, November 29, 2007

VIPI UNAMJUA MKALI WA KUNG-FU??

Ebwana nadhani wale makini wamekwisha gundua huyo ni nani ambaye anataka kuzungumziwa au sio?Kwa wale ambao wanaanza kujiuliza uliza hii inukuwaje tena?huyu jamaa anazungumzia mkaliwa kung-fu na wakati wako kibao wanaigiza filamu kibao,Hilo nalijua lakini watu wangu ukimzungumzia huyu ninaye mzungumzia ni kiboko,basi kama bado mnaumiza vichwa wale wenye kuwa na wasiwasi wala msipate tabu sana.Hata hivyo kabla sijawataji jina lake nikikwambia hivi nadhani utanipata,jamaa ameigiza filamu kama Shaolin temple 1&2 hiyo ni mwaka 1982 na 1983 pamoja na 3 mwaka 1986,Born to Defence nayo mwaka 1986,zingine ni kama Fist of legend(1994) na nyingine nyinngi pia Romeo must die(2000),The One na Kiss Of The Dragon mwaka 2001.Hero(2002),Fearless(2006) na The Warlords War(2007).Hizo movie sio kama nimewatajia zote watu wangu ni baadhi tu ya filamu alizocheza.Namzungumzia JET LEE na majina mengine kibao kama Lian Jie Li,Lianjie Li,Jet Li Lianjie,Jet Lee Lin-kit. Hayo yote ni majina yake. Jamaa alizaliwa tarehe 26 April 1963,huko Beijing,China.Huyo ndio mkali wa Kung Fu,Usikose habari zake pamoja na wengine wengi kwenye hii hii Blog yako kali ya filamu pamoja na waigizaji wa filamu hizo au sio.Kuwamakini kaa mkao wa kula.

No comments: