
Jamaa ni muigizaji mkali sana toka Hollywood,Jina lake kamili na
Mark Alan Dacascos, alizaliwa tarehe
26 February 1964, Honolulu, Hawaii, USA. Baba yake anaitwa
Al Dacascos ni
Mfilipino, mama yake mzazi anaitwa
Moriko McVey, lakini
Mark alilelewa na mama wa kambo aliyeitwa
Malia Bernal. Alianza kupata ushindi wa
karate na
kung fu akiwa na umri wa kati ya miaka 09 na 18.
Mark ameoa, mke wake anaitwa
Julie Condra na ana mtoto mmoja anaitwa
Makoa Dacascos ambae alizaliwa tarehe
31 December 2000, Oahu, Hawaii, USA.Kama kawaida wahenga wanasema mtoto wa nyoka ni nyoka, Dogo anaonekana atafuata nyayo za baba yake maana hadi sasa amekwisha igiza filamu inayoitwa
Final Approch (2006). Mark Dacascos mweyewe amekwisha igiza filamu(movie) nyingi sana kama vile
American Samurai(1992), Only the strong(1993), Crying Freeman(1995), Drive(1997), Final Approach(2006), Code Name.The Cleaner(2007), I am Omega(2007), The Legend of Bruce Lee ambayo inatoka
April mwaka huu
2008.Jamaa ana movie kibao.
Mark anaongea lugha ya
kiingereza, kijerumani na
kimandarin, pia viywaji vyake ni maji na chai tu.
Mark amekwisha wahi pata tuzo ya
Saturn Award mwaka
2002.Kwa ujumla
Mark Dacascos ni muigizaji mkali sana, tafuta na uangalie movie yake yoyote ile na utakuja niambia mwenyewe.Pia unaweza kubofya
hapa ili kupata mambo mengine ya
Mark. Msikose kufuatili mambo mengine kama haya yaani ni Utamuu! Ciao!!!
Pamojaa.