Monday, December 31, 2007

HUYU HAPA BRAD PITT MTU WANGU.

Watu wangu poleni sana kwa kusubiri kwa muda mrefu kidogo,lakini najua mnafahamu mambo ya sikukuu.kama mnavyojua wiki ya mwisho wa mwaka huwa karibu yote ni pilika za sikukuu.Tuyaache hayo.
Kama nilivyokuwa nimewaahidi lazima nitawaletea history ya muigizaji maarufu na mkali kutoka Hoollywood na huyu si mwingine ni Brad Pitt.
Kama nlivyowaambia mwanzo wakati nawapa story ya Angelina, hawa ni watu wilioowana na raha zaidi wanaigiza wote, check movie zao zimetulia.
Kwa kuanza jina kamili la huyu mshikaji ni William Bradley Pitt,alizaliwa tarehe 18 December 1963,Shawnee, Oklahoma, USA. Mama yake anaitwa Jane Etta Hillhouse na baba yake William(bill) Pitt. Pia kabla ya kuwa na Angelina alikuwa na mke wake aliyeitwa Jennifer Aniston ambae alimuoa tarehe 29 July na kumtaliki tarehe 02 October 2005 na ndipo alipo muoa Ange.Pamoja na kuwa muigizaji pia ni mtayarishaji wa filam,Jamaa alianza kupata umaarufu wake katika miaka ya tisini.Kama kawaida ameigiza movie kibao sana lakini ni baadhi ni kama Troy 2004, Mr& Mrs smith 2005, Babel 2006, Ocean Thirteen 2007 na zingine nyingi.Jamaa ana Historia ndefu sana ili nisiwachoshe pata hii kwa ufupi kabisa na usikose kufatilia issue kama hizi kibao za huyu na wengine. NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2008. Tchaooo.

No comments: